Friday, December 11, 2009

MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA IRINGA SOUTHERN HIGHLANDS YATESA IRINGA, RUVUMA YATOA VISINGIZIO VYA BARABARA.........




















Mkuu wa wilaya ya Mufindi Evarista Kalalu












Kulia ni Bw.Jackson Makwete mbunge wa jimbo la Njombe kaskazin na alipata kuwa waziri wa elimu akieleza changamoto zinazochangia shule za serikali kufanya vibaya ,
Mkurugenzi wa shule ya Southern Highlands Mafinga Bibi Mary Mungai

























Wahitimu wa darasa la saba katika shule ya Southern Highlands Mafinga
Afisa elimu mkoa wa Iringa Salum Maduhu ametangaza matokeo ya mtihani wa taifa wa darasa la saba leo mjini Njombe ambapo katika majina ya wanafunzi wavulana 10 bora kimkoa na shule walizotoka katika mabano alisema kuwa mwanafunzi Jared Kinzila aliyepata alama 226 (Southern Highlands ) atakwenda shule ya Iboru,Hildigard Mawondo alama 222(Southern Highlands atajiunga na shule ya sekondari ya Iyunga,Gift Nnko alama 221(southern Highlands) atajiunga na sekondari ya Kibaha,Honest Mwakabungu alama 220 amechaguliwa kujiunga na sekondari ya Kantalamba,Joshua Ngailo alama 220 (southern Highalnds ) atakwenda Moshi Tech na Grant Kilongo alama 220 (St.Benedict Njombe) amechanguliwa kujiunga na Ilboru.








Wasomaji wa mtandao huu wanatoa pongezi nyingi kwa uongozi wa shule ya Southern Highlands na wanafunzi wake pamoja na shule nyingine zote zilizofanya vyema katika matokeo haya.


Soma habari kamili hapa

Thursday, December 10, 2009

MATOKEO MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA KUTANGAZWA RASIMI


Waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Profesa Jumanne Maghembe kesho ijumaa anataraji kutangaza rasimi matokeo ya mtihani wa Taifa mwaka huu,matokeo ambayo yanasubiriwa kwa hamu kubwa na wazazi na wanafunzi wengi nchini ambapo kwa upande wa mkoa wa Iringa matokeo hayo yatatangazwa wilayani Njombe, pichani ni wanafunzi wa shule ya msingi Nyazwa Kilolo wakiutwanga usingizi wakati wakisubiri mwalimu kama ambavyo kamera yangu ilivyoweza kuwanasa

LEO NI SIKU YA KUPINGA UTATILI











Festo kaduma ni mlemavu wa ngozi (Albino) ambaye amelazimika kuishi kwa mganga wa kienyeji Dr Antony Mwandulami ili kuyanusuru maisha yake na waauwaji wa maalbino













Huyu pia ni mlemavu mkazi wa Njombe ambaye amekuwa akiishi kwa tabu nyingi,

Kumbuka leo ni siku ya kupinga ukatili duniani ,umejipanga vipi kupiga viti dhidi ya Ukatili katika eneo lako?

Wednesday, December 9, 2009

BREAKINGNewzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzz AJALI YAUA IRINGA





Basi la kampuni ya Sumry High Class lenye namba za usajili T 586 AVR Nissan likiwa linaning'inia hewani katika milima ya Kitonga barabara kuu ya Iringa -Dar es Salaam baada ya kugongana na magari mengine madogo mawili ,katika ajali hiyo kwenye basi hakuna mtu aliyepoteza maisha ila katika gari dogo watu wawili walikufa papo hapo (picha na Francis Godwin)











Wakazi wa eneo la Kitonga Iringa wakiangalia Tax yenye namba za usajili T 501 APX ikiwa imeharibika vibaya baada ya kugongana uso kwa uso na basi la Sumry leo mchana watu wawili waliokuwemo katika gari hii walikufa papo hapo(picha na Francis Godwin)

Pata habari kamili hapa


Tuesday, December 8, 2009

MIAKA 48 YA UHURU WA TANZANIA TUNAKWENDA AMA TUNARUDI?.....



Pichani waliokaa
mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dr Christine Ishengoma akiwa katika picha ya pamoja na chifu wa wangoni wa kwanza kulia Bw.Xavery zulu pamoja na viongozi wengine wa mkoa huo wakati wa maadhimisho ya uhuru yaliyokwenda sambamba na sherehe za makabidhiano ya makumbusho ya vita ya maji maji kati ya uongozi wa mkoa huo na bodi ya makumbusho Taifa sherehe zinazoelezwa kukosa mwitikio kwa wakazi wa mkoa huo (picha na mwandishi wa blog hii Ruvuma Bw Alpuas Mchucha)

Juu ni Rais wa Kwanza wa Tanzania ambaye ni mwasisi wa Taifa
















Rais mstaafu wa awamu ya Pili ya Tanzania














Rais Mstaafu wa awamu ya tatu ya Tanzania










Rais wa nne wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete ambaye anaonoza sasa .

*Je ? Miaka 48 ya Uhuru ni jambo gani ambalo watanzania tunaweza kujivunia?

*Unaonana kasi ya maendeleo ya Taifa toka Uhuru hadi sasa?
*Uadilifu kwa viongozi ukoje?
*Hali ya vyama vya siasa nchini ikoje? vipo kwa ajili ya maslahi ya wanachama ama viongozi wa vyama?
Unafikiri nini kifanyike ili kukabiliana na hali hiyo.

MUNGU WABARIKI VIONGOZI WA TANZANIA, MUNGU WABARIKI WATANZANIA, MUNGU IBARIKI TANZANIA ,MUNGU IBARIKI AFRIKA.

BREAKINGNEWzzzzzzzz MWALIMU NA FAMILIA YAKE HOI KWA KULA UGALI WENYE UTATA,MWANAFUNZI WA DARASA LA NNE AJINYONGA

















Bwa Anjelo Magedenge mkazi wa Pomelini Kilolo akiwa hajitambui hospitali ya mkoa wa Iringa baada ya kula chakula kinachosadikika kuwa na sumu
















Ndugu wa Anjelo wakiwa na mtoto Nanci katika wodi namba 8 wakiendelea kumuuguza mgonjwa huyo Anjelo ambaye hajitambui





Baba mzazi wa mwanafunzi Jenelari ambaye amekutwa kajinyonga katika mazingira tata akiwa na ndugu yake nje ya chumba cha kuhifadhia maiti hospitali ya mkoa wa Iringa .
Soma mikasa hii miwili hapa

videoSikiliza maelezo ya kifo cha Mwanafunzi Jenelari

BREAKINGNEZzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzBASI LA KAMPUNI YA HOOD LAPATA AJALI LAUA



Habari za uhakika za kusikitisha zilizotua katika mtandao huu hivi punde kutoka mkoani Morogoro zinadai kuwa basi la kampuni ya Hood linalofanya safari zake kati ya Dodoma na Mbeya limegongana uso kwa uso na gari ndogo katikati ya hifadhi ya Taifa ya Mikumi barabara kuu ya Morogoro -Iringa

Ajali hii ambayo imetokea mchana wa leo watu watatu ambao walikuwa katika gari ndogo ndio ambao wanaripotiwa kufa papo hapo huku abiri wa basi la Hood wakinusurika kifo.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Morogoro Bw Thobias Andengenya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo .
(Picha na maktaba )

TAARIFA ZA KUSIKITISHA IRINGA ZITAKUJIA HIVI PUNDE.......









Pamoja na serikali ya mkoa wa Iringa kupiga marufuku wazazi kuwatumikisha watoto katika ajira kama hizi ,agizo hili limeonyesha kukiukwa baada ya wazazi kuendelea kuwapa kazi kama hizi za kuponda na kukusanya kokoto watoto wao hapa ni eneo la milima ya Ipogoro leo mchana









Mchana huu Iringa kuna taarifa tata mbili ya kifo cha mtoto anayesadikika kujinyonga na watu kunywa sumu undani wake utautapa hivi punde

Monday, December 7, 2009

HIVI NDIVYO MTIKISIKO NA RADIO EBONY FM ULIVYOKUSANYA WATU IRINGA..........









MShiriki wamaisha Plus kutoka mkoa wa Iringa Shauri Mnyinga akiwaburudisha wakazi wa mkoa waIringa katika tamasha la Mtikisiko na Radio Ebony Fm lililofanyika jumapili katika uwanja wa Samora









Umati wa wakazi wa mkoa waIringa wakifuatilia tamasha hilo









Mambo yalivyozidi kupamba moto









Timu ya wasanii wa nyumbani Iringa ambao wanakuja juu kuliko TMK









Mambo ya taarabu ndani

Usikosekusoma gazeti la Tanzania Daima kesho kuona jinsi ambavyo bondia maarufu Rashid Matumla alivyoponea kufa kwa kipigo Iringa na Bondia Chupak Chipindu

BREAKINGNEWzzzzzzzzzz UMAGA AMEFARIKI DUNIA

bofya hapa

Sunday, December 6, 2009

MTIKISIKO NA RADIO EBONY FM WATIKISA MKOA WA IRINGA














Mwandishi Mwalubandu akionyesha umahiri wake katika kucheza









Mratibu wa Tamasha hilo Edo Bashiri akicheza na mmoja kati ya wasanii waliopamba tamasha hilo










Timu ya watangazaji mahiri wa Ebony Fm wakiwa katika picha ya pamoja na Bahath Alex (wa pili katikati)











Mtangazaji mwenye uwezo mkubwa radio Ebony Fm (87.5) Agnesy Andason (kushoto) akimkabidhi zawadi mnenguaji wa kujitolea Shakra ambaye alizawadiwa fedha sh.50,000 pamoja na zawadi nyingi mbali mbali










umati mkubwa wa watazamaji wa tamasha hilo










Hivi ndivyo ilivyokuwa ndani ya uwanja wa Samora








SOPHIA SIMBA ASEMA HANA UGOMVI WA ANNE KILANGO.................







Mwenyekiti wa UWT Taifa Sophia Simba akitoa ufafanuzi leo mbele ya waandishi wa habari juu ya tuhuma mbali mbali zinazoelekezwa kwake





Anne Kilango ,mbunge wa jimbo la Same Mashariki





Mwenyekiti wa UWT Sophia Simba akitoa ufafanuzi leo mbele ya waandishi wa habari Iringa



















Mwenyekiti wa UWT Taifa mama Sophia Simba leo amefanya mkutano na waandishi wa habari mkoani Iringa na kujibu tuhuma mbali mbali zinazoendelea kuelekezwa kwake ,katika mahojiano hayo amekanusha madai ya kuwepo na mgogoro kati yake ya mbunge wa Same Mashariki mama Anne Kilango na kuwa yeye hana ugomvi wowote na mbunge huyo ila anachotambua yeye na KIlango ni marafiki wakubwa,

Pia amesema kuwa hakuna kundi linalompinga Rais Jakaya Kikwete zaidi ya kijikundi cha watu wasio zidi 20 kinachoongozwa na kigogo mmoja ambaye amekuwa akitumiwa na baadhi ya watu wa nchi za magharibi wanaopinga CCM kuendelea kuongoza.


Kuhusu yeye kuwa mtetezi wa mafisadi Simba amesema kuwa yeye si mtetezi wa mafisadi ila ni msimamizi wa sheria na utawala bora

Ili kujua undani zaidi wa mahojiano hayo soma gazeti la Tanzania daima leo ama soma hapa

Saturday, December 5, 2009

BREAKINGNEWzzzzzzzzzzzzzzzzzzz GARI LA WAJUMBE WA UWT LAGONGA NA KUUA WATANO LILIKUWA LIKIENDA KUMPOKEA SOPHIA SIMBA..


Ziara ya mwenyekiti wa UWT Taifa Sophia Simba ambaye ni waziri wa nchi ofisi ya Rais utawala bora ,ambaye yupo mkoani Iringa imeingia dosari kubwa baada ya gari la wajumbe wa UWT wilaya ya Makete kuwagonga watu watano na kusababisha vifo vyao papo hapo .

Ajali hiyo imetokea leo asubuhi ambapo wajumbe hao walikuwa wakielekea Njombe kwa ajili ya mkutano kati yao na mwenyekiti wa UWT Taifa ambaye alikuwa akitokea mjini Iringa

Habari kamili utaipata katika gazeti la Tanzania Daima kesho ama katika mtandao huu

Friday, December 4, 2009

MENEJA WA RADIO COUNTRY FM BIBI NEEMA KINDOLE LEO ANAADHIMISHA SIKU YA KUZALIWA.


Wasomaji wa mtandao huu wanaungana na mmiliki wa mtandau huu Bw Francis Godwin pamoja na chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa,wafanyakazi wote wa Radio Country Fm kumpongeza meneja wa Radio Country Fm (88.5) Iringa Bibi Neema Kindole pichani kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa na kutimiza miaka 27,Neema alizaliwa tarehe 5/12/1982.

Neema pamoja na kuwa meneja pia ni mmoja kati ya watangazaji maarufu katika radio za mikoa ya nyanda za juu kusini na utangazaji wake umekuwa ukivutia wasikilizaji wengi na hata kuendelea kuwa na shauku ya kutaka vipindi vyake kuendelea hata kama muda umekwisha .

Zawadi ya moja kwa moja ya kutoa kwake bado sijapata kuiandaa ila kubwa kuliko yote napenda kuzidi kumwombea kwa mwenyezi Mungu uzima na afya tele na kumpa nguvu ya kulitumikia Taifa kwa kipaji chake alichompa.

TASWA IRINGA YAANDAA MASHINDANO YA RIADHA KWA WANAWAKE WANENE NA WANAUME WENYE VITAMBI, ILI KUMCHANGIA MLEMAVU


Chama cha waandishi wa Habari za michezo Tanzania (TASWA) mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na Blog hii ,Radio Country Fm (88.5 Iringa ) IMTV wameandaa mchezo wa hisani kwa ajili ya kumchangia fedha za mtaji mlemavu Yolanda Mbangile ambaye ametelekezwa baada ya kuzalishwa watoto wawili na mfanyabiashara ,Asha kalani pichani ni mshiriki namba moja.


Michezo itakayoshindaniwa ni mpira wa miguu kati ya TASWA Iringa na timu ya wanawake Mufindi na Manispaa ya Iringa na mashindano ya kukimbia mita 100 na kufukuza kuku kwa wanaume wenye vitambi na wanawake wanene .
Wenye sifa zilizotajwa wapige simu namba 0754 026 299 au 0717797366











Asha All (kushoto) mshiriki namba mbili














Kalaleta Fuime mshiriki namba tatu














Ameria Galinoma mshiriki namba nne.

Wadhamini wa tamasha hilo litakalofanyika Desemba 13 siku ya jumapili mwaka huu ni chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IPC) IMTV ,Radio Country FM, Da mariam Shop ,Kamanda wa umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) Iringa mjini BW Eferehem Mhule, Shule ya kimataifa ya Star Iringa,CCM mkoa wa Iringa na wengine wanakaribishwa
video SIKILIZA MAJINGAMBO YA MSHIRIKI MNENE KULIKO WENZAKE JINSI ALIVYOJIANDAA KUSHINDA.

SOPHIA SIMBA AFYATUKA AGEUKA MBOGO KWA VYOMBO VYA HABARI ......................



Mwenyekiti wa UWT Taifa Mh.Sophia Simba ambaye ni waziri wa nchi ofisi ya rais na Utawala bora akiwahutubia wanawake wa UWT mkoa wa Iringa leo ambapo ameweza kukana tuhuma dhidi yake
Umati wa wana wake wa UWT mkoa wa Iringa wakimpokea mwenyekiti wao Sophia Simba leo eneo la Igumbilo nje kidogo na mji wa Iringa ambako maandamano makubwa yamefanywa na wanawake hao




Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Iringa Zainabu Mwamwindi (wa pili kulia ) akiwa na viongozi wenzake wakimpokea mwenyekiti wa UWT Taifa Sophia Simba ( wa tatu kulia) leo
Mwenyekiti huyo wa Taifa leo ameshindwa kujizuia kukana tuhuma dhidi yake na kuwa wanawake wasidanganywe na vyombo vya habari soma hapa

Thursday, December 3, 2009

LEO NI SIKU YA WALEMAVU DUNIANI,MFANYABIASHARA ADAIWA KUZAA NA MWANAFUNZI MLEMAVU NA KUMKIMBIA.........












Mlemavu Yolanda ambaye anadaiwa kutelekezwa na mfanyabiashara baada ya kumzalisha watoto wawili .









Yolanda akiwa Neema Craft ambako anafanya kazi ya kushona










Mlemavu akiendelea na shughuli zake









Mlemavu Claud akipanga nguo kwa ajili ya kuziuza









Msamalia mwema akimsaidia shilingi 5000 mmoja kati ya walemavu wanaofanya kazi ya kuomba misaada eneo la Posta mjini Iringa


WAKATI leo ni siku ya maadhimisho ya watu wenye ulemavu duniani ,mfanyabiashara maarufu mkoani Iringa anadaiwa kumzalisha watoto wawili mlemavu wa viungo aliyekuwa akisoma kidato cha pili katika sekondari ya Lugalo Iringa kuhama mkoa.

Mfanyabiashara huyo anadaiwa kumdanganya mlemavu huyo kuwa angemsomesha hadi chuo kikuu iwapo na asingependa mtu yeyote hata ndugu kujua kama yeye ana mahusiano na mlemavu huyo ila baada ya kumpa mimba alihama mkoa na kukimbilia mkoa wa Arusha ambako anaendelea na biashara zake hadi sasa,kumbuka leo ni siku ya walemavu duniani je?nini kifanyike kuwalinda walemavu dhidi ya unyama wanaoendelea kutendewa? Je? Yolanda anapaswa kusaidiwa kuendelea na Masomo?

Usikose gazeti la Tanzania Daima kesho ama soma hapa

Wednesday, December 2, 2009

DR MSHINDO MSOLLA AWALIZA WAOMBOLEZAJI ............











Waziri wa mawasiliano ,Sayansi na Teknolojia Prof.Peter Msolla (katikati) akisaidiana na Bw.Mnyanyi kuweka sawa na mwili wa mama mzazi wa Dr Mshindo Msolla huku kulia ni Dr Mshindo mwenyewe akiangua kilio kwa huzuni












Dr Mshindo (kulia) akilia kwa huzuni huku pembeni ni waziri MSolla ambaye muda wote alikuwa akimponza mdogo wake atulie kulia
videoSikiliza salamu wa waziri Msolla hapa,pia usikose picha zaidi za shughuli za mazishi kesho katika mtandao wa www.matukiodaima.blogspot.com

UWT IRINGA YAAMUA KUVUNJA UKIMYA DHIDI YA ANNA KILANGO


PAMOJA na mbunge wa jimbo la Same Mashariki Bi.Anna Kilango Malecela (pichani)kujiita ni mmoja kati ya wanaharakati wa vita dhidi ya ufisadi na hata kuendelea kuukosoa uongozi wa jumuiya ya wanawake Tanzania (UWT) chini ya mwenyekiti wake Sophia Simba ,UWT mkoa wa Iringa imeamua kujibu mapigo kwa mbunge huyo kuwa Simba ni mchapakazi makini na halingani na Kilango amelenga kuyumbisha UWT na CCM.

Hivyo UWT mkoa wa Iringa imemtaka mbunge Kilango kama ni kiongozi mwenye mapenzi mema na jumuiya hiyo na CCM kuendelea kuiheshimu UWT na mwenyekiti huyo pamoja na CCM na kinyume cha hapa wanawake hawatakuwa tayari kuendelea kunyamaza kwa mtu mmoja kuendelea kuwavuruga.


Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Iringa na mjumbe wa baraza kuu la UWT Taifa Bi Zainabu Mwamwindi alitoa onyo hilo wakati akielezea maandalizi makubwa ambayo wanawake mkoa wa Iringa wameandaa (Ijumaa) kwa ajili ya mwenyekiti wao Taifa Bi Simba ambaye anafanya ziara yake mkoani Iringa.

Undani wa habari hii utaupata ndani ya gazeti la Taifa Tanzania Ijumaa hii

Tuesday, December 1, 2009

MSIBA IRINGA :MAMA MZAZI WA ALIYEKUWA KOCHA WA TIMU YA TAIFA KILIMANJARO STARS AMEFARIKI DUNIA










Maombolezi ya kifo cha mama wa Dr Msolla









Ndugu na jamaa wa waziri wa mawasiliano sayansi na Teknolojia Prof.Peter Msolla ambaye ni mbunge wa jimbo la Kilolo Iringa wakiwa nje ya chumba cha maiti katika hospitali ya mkoa wa Iringa wakisubiri kuaga mwili wa mama mdogo na mbunge huyo na mama mzazi wa aliyekuwa kocha mkuu wa Kilimanjaro Stars Dr Mshindo Msolla aliyefariki jana Desemba mosi








Ndugu na wananchi wa jimbo la Kilolo wakiwa katika maombolezo ya kifo cha mama mdogo wa mbunge wa jimbo la Kilolo Prof Msolla










Marehemu Veronica Kapone (80) anatarajia kuzikwa leo mchana kijijini kwake Image wilaya ya Kilolo Iringa ,wasomaji wa mtandao huu na mmiliki wanaungana na ndugu na jamaa wa Dr Msolla katika kuomboleza msiba huu na kumwomba mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi Amina

Nb.Taarifa zaidi za mazishi na matukio yatakayojiri katika msibu huu utayapata jioni ya leo katika mtandao wa www.matukiodaima.blogspot.com