Mkuu wa wilaya ya Mufindi Evarista Kalalu
Kulia ni Bw.Jackson Makwete mbunge wa jimbo la Njombe kaskazin na alipata kuwa waziri wa elimu akieleza changamoto zinazochangia shule za serikali kufanya vibaya ,
Mkurugenzi wa shule ya Southern Highlands Mafinga Bibi Mary Mungai

Wahitimu wa darasa la saba katika shule ya Southern Highlands Mafinga
Afisa elimu mkoa wa Iringa Salum Maduhu ametangaza matokeo ya mtihani wa taifa wa darasa la saba leo mjini Njombe ambapo katika majina ya wanafunzi wavulana 10 bora kimkoa na shule walizotoka katika mabano alisema kuwa mwanafunzi Jared Kinzila aliyepata alama 226 (Southern Highlands ) atakwenda shule ya Iboru,Hildigard Mawondo alama 222(Southern Highlands atajiunga na shule ya sekondari ya Iyunga,Gift Nnko alama 221(southern Highlands) atajiunga na sekondari ya Kibaha,Honest Mwakabungu alama 220 amechaguliwa kujiunga na sekondari ya Kantalamba,Joshua Ngailo alama 220 (southern Highalnds ) atakwenda Moshi Tech na Grant Kilongo alama 220 (St.Benedict Njombe) amechanguliwa kujiunga na Ilboru.
Wasomaji wa mtandao huu wanatoa pongezi nyingi kwa uongozi wa shule ya Southern Highlands na wanafunzi wake pamoja na shule nyingine zote zilizofanya vyema katika matokeo haya.
Soma habari kamili hapa









Dar Es Salaam Time