January 27, 2012

Breakingnewsssss Msafara wa makamu wa Rais wapata ajali WAUA

Msafara wa Makamu wa Rais Dokta MOHAMMED GHARIB BILAL umepata ajali baada ya gari lililokuwa limebeba Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia kupinduka katika eneo lenye mteremko mkali la Nduru-Mombo Wilaya Korogwe Mkoani Tanga.

Kufuatia ajali hiyo Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya cha Magungu Dokta RASHID SAID amethibitisha kutokea kwa vifo Viwili vya askari polisi huku akisisitiza kuwa hali za askari Wanne waliojeruhiwa katika ajali hiyo bado si nzuri.

Mwandishi wa habari wa Uhuru FM aliyekuwepo kwenye msafara huo amesema msafara huo ulikuwa unatokea Wilayani Lushoto kwenda Hale Wilayani Korogwe kwa ajili ya mapumziko ya Makamu wa Rais ambaye yupo Mkoani Tanga kwa ajili ya ziara ya kikazi.

Gari lililohusika katika ajali hiyo ni lenye namba za usajili PT-2000 ambalo lilikuwa nyuma ya msafara huo wa Makamu wa Rais.

Miili ya askari hao waliokufa imehifadhiwa katika Kituo cha Afya cha Magungu.

0 Maoni: